Wednesday, November 30, 2011

MOTO! MOTO! MOTO! MOTO! MOTO! MBEYA

BAADA YA MASOKO MAWILI KUUNGUA MBEYA, HAYA NDIYO YANAYOENDELEA


watoto+tafuta.JPG
Watoto wakitafuta sarafu eneo lilipoungua soko la Sido Mwanjelwa Mbeya juzi.
jenga+tena.JPG
Ujenzi ukiendelea eneo lilioungua soko la Sido Mwanjelwa Mbeya.
uza+tena.JPG
Baada ya kuunguliwa akina mama wanaendelea kujitafutua riziki pambeni kidogo mwa soko hilo
akiangalia+soko+Mbowe.JPG
Chadema ilipotua eneo la ajali ya Mwanjelwa baada ya siku moja moto kuzimwa.
Mbowe+akimnadi+mgombea+Majengo+Mbeya.JPG

Hatimaye siasa zikandelea kata ya majengo Jijini Mbeya.  PICHA KUTOKA MTANDAONI




Usiku wa kuamkia leo huko jijini Mbeya,Moto ambao haukufahamika chanzo chake uliteketeza soko dogo lililopo maeneo ya Forest ya zamani karibu na Chuo kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu huria matawi ya Jijini Mbeya na kusababisha mabada kadhaa kuteketea kwa moto ambao uliwahiwa na kikosi cha zima moto cha mkoa wa Mbeya.
Mdau alietuletea picha hizi ambaye alifika eneo la tukio mapema leo asubuhi na kukuta moto umefanikiwa kuzimwa katika vibanda hivyo vilivyokuwepo sokoni hapo na kutuletea taswira hizi za mabaki ya mabanda yaliyoungua moto katika soko hilo yakiendelea kufuka moshi.

Mashuhuda waliokuwepo maeneo ya jirani na soko hilo walisema Moto huo ulianza majira ya saa 9:00 kamili usiku na muda si mrefu taarifa ziliwafikia kikosi cha Zimamoto na wao walifika eneo la tukio dakika 10 baadae na kufanikiwa kuuzima moto huo bila hata ya maigizo yao ya kila siku ya kufika eneo la tukio bila ya kuwa na maji au kuharibika kwa gari wakati wakiwa kwenye tukio.maswali mengi sana yamekuwa yakiulizwa hivi sasa Jijini Mbeya juu ya majanga ya moto katika masoko ya Mbeya kila siku na kwanini tahadhari hazichukuliwi mapema na wakati hali hiyo imekuwa ikijirudia mara kwa mara??


No comments:

Post a Comment