Monday, March 19, 2012

LOVE BETWEEN BLUE AND WAHIDA



BLU, WAHIDA PENZI MIAKA 7

                 Herry Samir ‘Blu’.
             Wahida.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Herry Samir ‘Blu’ amefunguka kuwa amekaa kwenye uhusiano wa kimapenzi na demu aliyemtaja kwa jina la Wahida kwa miaka saba hivyo hawezi kumuacha kamwe.
Akizungumza na Ijumaa juzikati Blu alisema, yeye na Wahida wametoka mbali na wamevumiliana kwa mengi hivyo kumuacha itakuwa ni kosa kubwa katika maisha yake.
Alisema walikuwa wakiendesha uhusiano wao kwa siri sana na ndiyo maana hawakuwa wamevishana pete lakini sana anaamini ni muda muafaka wa kufanya hivyo.
“Nampenda sana Wahida, ni msichana wa maisha yangu na siku si nyingi nitadhihirisha upendo wangu kwake kwa kumvisha pete ya uchumba,” alisema Blu.
Alipobanwa juu ya tetesi zilizozagaa kitaani kuwa ana kidemu kingine kinamzingua mbali na Wahida, Blu alisema hayo ni maneno ya watu tu licha ya kwamba kuna wengi wanamshobokea.

No comments:

Post a Comment